Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Marko 12:6-11

Marko 12:6-11 NENO

“Mwenye shamba alikuwa bado na mmoja wa kumtuma, mwanawe aliyempenda. Hatimaye akamtuma akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’ “Lakini wale wapangaji wakasemezana pamoja, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, nao urithi utakuwa wetu.’ Hivyo wakamchukua na kumuua, wakamtupa nje ya lile shamba la mizabibu. “Sasa basi yule mwenye shamba atafanya nini? Atakuja na kuwaua hao wapangaji, kisha atawapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu. Je, hamjasoma andiko hili: “ ‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni; Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni la kushangaza machoni petu’?”