Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yeremia 4:1-9

Yeremia 4:1-9 NENO

“Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema BWANA. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga, ikiwa utaapa katika kweli, kwa haki na kwa unyofu, ‘Hakika kama BWANA aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye, na ndani yake watajitukuza.” Hili ndilo asemalo BWANA kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba. Jitahirini katika BWANA, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima. “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu, useme: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye ngome!’ Inueni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.” Simba ametoka nje ya pango lake, mwangamizi wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo. Hivyo vaeni magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya BWANA haijaondolewa kwetu. “Katika siku ile,” asema BWANA “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”