Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mwanzo 27:14-20

Mwanzo 27:14-20 NENO

Kwa hiyo alienda akawaleta, akampa mama yake, naye Rebeka akaandaa chakula kitamu, kile alichokipenda baba yake. Kisha Rebeka akachukua nguo nzuri za Esau mwanawe wa kwanza, alizokuwa nazo nyumbani, akamvika Yakobo mwanawe mdogo. Pia akamfunika mikononi na sehemu laini ya shingo kwa ngozi za mbuzi. Hatimaye akampa Yakobo hicho chakula kitamu pamoja na mkate aliouoka. Yakobo akaenda kwa baba yake, akasema, “Baba yangu.” Akajibu, “Naam, mwanangu. Wewe ni nani?” Yakobo akamwambia baba yake, “Mimi ni Esau mzaliwa wako wa kwanza. Nimefanya kama ulivyoniambia. Tafadhali uketi, ule sehemu ya mawindo yangu ili unibariki.” Isaka akamuuliza mwanawe, “Umepataje mawindo haraka hivi, mwanangu?” Akajibu, “BWANA Mungu wako amenifanikisha.”