Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

2 Samweli 7:1-11

2 Samweli 7:1-11 NENO

Baada ya mfalme kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, naye BWANA akiwa amempa amani pande zote kutoka kwa adui zake, akamwambia nabii Nathani, “Mimi hapa ninaishi katika jumba la kifalme la mwerezi, wakati Sanduku la Mungu limebaki katika hema.” Nathani akamjibu mfalme, “Lolote ulilo nalo moyoni, endelea ukalifanye, kwa maana BWANA yu pamoja nawe.” Usiku ule neno la BWANA likamjia Nathani, kusema: “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo BWANA: Je, ewe ndiwe wa kunijengea mimi nyumba ili nikae ndani yake? Sijakaa ndani ya nyumba tangu siku niliyowaleta Waisraeli kutoka Misri hadi leo. Nimekuwa nikitembea kutoka mahali pamoja hadi mahali pengine na hema kama makao yangu. Popote nilipotembea pamoja na Waisraeli wote, je, nimewahi kumwambia kiongozi wao yeyote niliyemwamuru kuwachunga watu wangu Israeli, “Kwa nini hujanijengea nyumba ya mwerezi?” ’ “Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo BWANA wa majeshi: Nilikutoa malishoni na kutoka kulisha mifugo, ili uwaongoze watu wangu Israeli. Nimekuwa pamoja nawe popote ulipoenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani. Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali niwapande humo ili wawe na nyumbani kwao wenyewe wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawatesa tena, kama walivyofanya mwanzoni, na kama walivyofanya tangu mwanzo wakati nilipowaweka viongozi juu ya watu wangu Israeli. Pia nitawapa amani mbele ya adui zenu wote. “ ‘BWANA akuambia kwamba BWANA mwenyewe atakujengea nyumba.