2 Wakorintho 5:18-19
2 Wakorintho 5:18-19 NENO
Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kupitia kwa Yesu Kristo, na kutupatia sisi huduma ya upatanisho: kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho.







