Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Wafalme 20:35-43

1 Wafalme 20:35-43 NENO

Kwa neno la BWANA, mmoja wa wana wa manabii akamwambia mwenzake, “Nipige kwa silaha yako,” lakini yule mtu akakataa. Kwa hiyo yule nabii akasema, “Kwa sababu hukumtii BWANA, mara tu tutakapoachana utauawa na simba.” Na baada ya yule mtu kuondoka, simba akatokea na kumuua. Nabii akamkuta mtu mwingine na kumwambia, “Nipige, tafadhali!” Kisha yule mtu akampiga na kumjeruhi. Ndipo nabii akaenda na kusimama barabarani akimsubiri mfalme. Akajibadilisha kwa kushusha kitambaa cha kichwani mwake hadi kwenye macho. Mfalme alipopita pale, yule nabii akamwita, “Mtumishi wako alienda vitani mahali vilikuwa kali. Mtu mmoja akanijia akiwa na mateka, akasema, ‘Mlinde mtu huyu. Akitoroka, itakuwa uhai wako kwa uhai wake, ama utalipa talanta ya fedha.’ Mtumishi wako alipokuwa na shughuli nyingi hapa na pale, yule mtu akatoweka.” Mfalme wa Israeli akasema, “Hiyo ndiyo hukumu yako. Wewe umeitaja mwenyewe.” Kisha yule nabii akajifunua macho yake haraka, na mfalme wa Israeli akamtambua kama mmoja wa manabii. Akamwambia mfalme, “Hivi ndivyo asemavyo BWANA: ‘Umemwacha huru mtu niliyekusudia afe. Kwa hivyo ni uhai wako kwa uhai wake, watu wako kwa watu wake.’ ” Kwa uchungu na hasira, mfalme wa Israeli akaenda kwenye jumba lake huko Samaria.