Ndiye, Mungu aliyemtoa, kusudi wenye kumtegemea wajipatie Kiti cha Upozi katika damu yake; hapo ndipo, alipoonyesha, wongofu wake ulivyo, akiwaondolea makosa ya kale, ambayo Mungu alikuwa akiyavumilia. Hivi ndivyo, alivyouonyesha siku hizi za sasa wongofu wake kuwa hivyo: Mwenyewe ni mwongofu, tena mwenye kumtegemea Yesu humpa wongofu.