1
Luka 9:23
Swahili Roehl Bible 1937
SRB37
Akawaambia wote: Mtu akitaka kunifuata mimi ajikataze mapenzi yake, ajitwishe kila siku nao msalaba wake, kisha anifuate!
Linganisha
Chunguza Luka 9:23
2
Luka 9:24
Maana mtu anayetaka kuiokoa roho yake ataiangamiza. Lakini mtu atakayeiangamiza roho yake kwa ajili yangu mimi, huyo ataiokoa.
Chunguza Luka 9:24
3
Luka 9:62
Yesu akamwambia: Mtu ashikaye jembe mkononi na kuvitazama vya nyumba, huyo hatauweza ufalme wa Mungu.*
Chunguza Luka 9:62
4
Luka 9:25
Kwani mtu vinamfaa nini, avichume vya ulimwengu wote, akijiangamiza mwenyewe, au akiponzwa navyo?
Chunguza Luka 9:25
5
Luka 9:26
Kwani mtu atakayenionea soni mimi na maneno yangu, basi, naye Mwana wa mtu atamwonea soni huyo atakapokuja mwenye utukufu wake yeye na wa Baba yake na wa malaika watakatifu.*
Chunguza Luka 9:26
6
Luka 9:58
Yesu akamwambia: Mbweha wanayo mapango, nao ndege wa angani wanavyo vituo, lakini Mwana wa mtu hana pa kukilazia kichwa chake.
Chunguza Luka 9:58
7
Luka 9:48
akawaambia: Mtu atakayempokea kitoto huyu kwa Jina langu hunipokea mimi. Tena akinipokea mimi humpokea yule aliyenituma mimi. Kwani aliye mdogo kwenu ninyi wote, huyo ndiye mkuu.
Chunguza Luka 9:48
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video