1
Rom 2:3-4
BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA
SCLDC10
Lakini wewe rafiki unayewahukumu wale wanaofanya mambo kama hayo hali wewe pia unayafanya, je unadhani utaiepa hukumu ya Mungu? Au labda unaudharau wema wake mkuu, uvumilivu wake na saburi yake, bila kutambua kwamba wema wake huo una shabaha ya kukuongoza upate kutubu?
Linganisha
Chunguza Rom 2:3-4
2
Rom 2:1
Basi, rafiki, kama unawahukumu wengine, huwezi kamwe kujitetea, hata kama wewe ni nani. Kwa maana, kwa kuwahukumu wengine, unajilaani wewe mwenyewe kwa vile nawe unayafanya mambo yaleyale unayohukumu.
Chunguza Rom 2:1
3
Rom 2:11
Maana Mungu hambagui mtu yeyote.
Chunguza Rom 2:11
4
Rom 2:13
Maana sio wanaosikia sheria ndio walio waadilifu mbele ya Mungu, ila wenye kuitii sheria ndio watakaokubaliwa kuwa waadilifu.
Chunguza Rom 2:13
5
Rom 2:6
Siku hiyo Mungu atamlipa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
Chunguza Rom 2:6
6
Rom 2:8
Lakini wale wengine wenye ubinafsi, wenye kukataa mambo ya haki na kufuata uovu, wataangukiwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
Chunguza Rom 2:8
7
Rom 2:5
Lakini unao ugumu na ukaidi wa moyo, na hivyo unajirundikia adhabu kwa siku ile ya ghadhabu wakati hukumu ya haki ya Mungu itakapodhihirishwa.
Chunguza Rom 2:5
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video