1
1 Wathesalonike 5:16-18
BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA
SCLDC10
Furahini daima, salini kila wakati na kuwa na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
Linganisha
Chunguza 1 Wathesalonike 5:16-18
2
1 Wathesalonike 5:23-24
Mungu mwenyewe anayetupatia amani awatakase nyinyi kabisa kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu – roho, mioyo na miili yenu – mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye anayewaita nyinyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:23-24
3
1 Wathesalonike 5:15
Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:15
4
1 Wathesalonike 5:11
Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana nyinyi kwa nyinyi, kama mnavyofanya sasa.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:11
5
1 Wathesalonike 5:14
Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:14
6
1 Wathesalonike 5:9
Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo
Chunguza 1 Wathesalonike 5:9
7
1 Wathesalonike 5:5
Nyinyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
Chunguza 1 Wathesalonike 5:5
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video