BWANA asema, “Siku zinakuja,
nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki,
Mfalme atakayetawala kwa hekima,
na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
Katika utawala wake, Yuda ataokolewa,
na Israeli ataishi salama.
Hili ndilo jina atakaloitwa:
BWANA ni Haki Yetu.”