Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Mwa 12:2

Mwanamume Wa Kifalme
Siku 5
Katika historia yote, Mungu daima amewatafuta na kuwatumia wanaume kuendeleza ajenda ya Ufalme wake. Shetani anajua hili, ndiyo maana anataka kuwafungia na kuwahasi wanaume. Ulimwengu wetu unaendelea ukizorota kwa sababu wanaume hawapatikani popote. Ni wakati wa wanaume kusimama kidete. Katika mpango huu wa kusoma wa siku tano, Daktari Tony Evans atakupeleka kwenye safari ya kufanyika mwanamume ambaye Mungu alikuumba uwe.

Mwongozo wa KiMungu
Siku 7
Kila siku tunafanya maamuzi ambayo yana unda hadithi ya maisha yetu. Maisha yako yangekuwaje kama ungekuwa bingwa wa kufanya maamuzi? Kwenye Mpango wa Biblia wa Mwongozo wa kimungu, mwandishi mzuri wa New York Times na Mchungaji Kiongozi, Craig Groeschel, anakutia moyo na kanuni saba kutoka kwenye kitabu chake cha Mwongozo wa Kimungu ili kukusaidia kupata busara ya Mungu kwa maamuzi yako kila siku. Gundua mwongozo wa kiroho unaohitaji ili kuishi hadithi ya maisha ya kumheshimu Mungu utakayopenda kuhadithia.

Nenda Tenda Sema Toa: Uhuru wa Kujisalimisha kwa Yesu
Siku 7
Kujisalimisha kwa Yesu ni tukio kubwa maishani. Lakini uamuzi huu unamaanisha nini na tutauishi vipi kila siku? Uamuzi ni wa mambo makubwa ya maisha pekee, ama wacha Mungu kupita kiasi? Woga, makosa yaliyopita, na kutoelewa vinaweza kutuzuia. "Nenda Tenda Sema Toa" ni ahadi/sala ambayo inafunua jinsi utakavyochukua hatua zinazofuata katika safari yako ya kiroho. Pata uhuru unaotokana na kumfuata Yesu.

Utiifu
Wiki 2
Yesu mwenyewe alisema ambaye yeyote anaye mupenda atatii mafundisho Yake. Haijalishi gharama yake kwa kila mutu, utiifu wetu ndio wa muhimu kwa Mungu. "Utiifu" Mpango wa usomaji inachukua jinsi maandiko yanavyo sema kuhusu utiifu: Namna gani kulinda musimamo ya uadilifu, jukumu ya rehema, namna gani utiifu hutufanya huru na hubariki maisha yetu, na kadhalika.