1
Wakolosayi 3:13
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Muvumiliane na kusameheana ninyi kwa ninyi wakati wowote mutu anapokuwa na neno la kumushitaki mwingine. Munapaswa kusameheana kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
तुलना
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:13
2
Wakolosayi 3:2
Mushugulikie sana mambo yanayokuwa juu, lakini musishugulikie mambo yanayokuwa katika dunia.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:2
3
Wakolosayi 3:23
Na kila kitu munachofanya, mukifanye kwa moyo wenu wote, kama vile wenye kumutumikia Bwana wala si watu.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:23
4
Wakolosayi 3:12
Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:12
5
Wakolosayi 3:16-17
Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho. Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:16-17
6
Wakolosayi 3:14
Zaidi ya mambo haya yote, mukuwe na upendo, maana upendo unaunganisha kila kitu katika umoja unaokuwa mukamilifu.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:14
7
Wakolosayi 3:1
Kwa kuwa mumefufuliwa pamoja na Kristo, mutafute mambo yanayokuwa juu, pahali Kristo anapoikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:1
8
Wakolosayi 3:15
Amani ya Kristo itawale katika mioyo yenu; maana ni kwa ajili ya hiyo ninyi mumeitwa kuwa katika mwili mumoja. Mukuwe wenye shukrani.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:15
9
Wakolosayi 3:5
Basi mutupilie mbali mambo yote ya kidunia yanayokuwa ndani yenu: uasherati, uchafu, nia mbaya, tamaa mbaya na tamaa ya mali inayokuwa sawa vile kuabudu sanamu.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:5
10
Wakolosayi 3:3
Kwa maana ninyi mumekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:3
11
Wakolosayi 3:8
Lakini sasa mutupilie mbali mambo haya yote: kasirani, chuki, uovu, masingiziano na musiseme neno lolote baya.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:8
12
Wakolosayi 3:9-10
Musiambiane uongo ninyi kwa ninyi, kwa maana mumeondoa utu wenu wa zamani pamoja na matendo yake na kuvaa utu mupya. Utu ule unaendelea kufanywa upya kila mara kufuatana na mufano wa Mungu anayekuwa muumba wake, kusudi mupate kumujua hakika.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:9-10
13
Wakolosayi 3:19
Waume muwapende wake wenu nanyi musiwatendee kwa ukali.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:19
14
Wakolosayi 3:20
Watoto muwatii wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana jambo hili linamupendeza Bwana.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:20
15
Wakolosayi 3:18
Wake muwatii waume wenu kama vile inavyostahili mbele ya Bwana.
अन्वेषण गर्नुहोस् Wakolosayi 3:18