INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA TISAExemple

YESU AMPONYA MWANAMKE ALIYEJIKUNYATA
"Basi Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo siku ya Sabato.Wakati uo huo akaja mwanamke mmoja aliyekuwa na pepo mchafu, naye alikuwa amepinda mgongo kwa muda wa miaka kumi na minane, wala alikuwa hawezi kunyoka wima."
Yesu alipomwona, akamwita akamwambia, “Mwanamke, uwe huru, umepona ugonjwa wako.”
Yesu alipomwekea mikono yake, mara akasimama wima akaanza kumtukuza Mungu.
Lakini mkuu wa sinagogi, akakasirika kwa sababu Yesu alikuwa ameponya mtu siku ya Sabato. Kwa hiyo mkuu wa sinagogi akaendelea kuuambia ule umati wa watu,
“Kuna siku sita ambazo watu wanapaswa kufanya kazi, katika siku hizo, njoni mponywe, lakini si kuja kuponywa siku ya Sabato.”
Lakini Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Je, kila mmoja wenu hamfungulii ng'ombe wake au punda wake kutoka zizini akampeleka kumnywesha maji siku ya Sabato?
Je, huyu mwanamke, ambaye ni binti wa Abrahamu, aliyeteswa na Shetani akiwa amemfunga kwa miaka yote hii kumi na minane, hakustahili kufunguliwa kutoka katika kifungo hicho siku ya Sabato?”
Aliposema haya, wapinzani wake wakaaibika, lakini watu wakafurahi kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyoyafanya.
Écritures
À propos de ce plan

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana
More
Plans suggérés

ILLIMITÉ

Les portes démoniaques

Enveloppé : Une réflexion sur les promesses de Dieu au Psaume 91

Dieu veut vous parler !

Une Randonnée Biblique en Montagne

Journée mondiale de prière pour les universitaires: Guide de prière de 40 jours

Transcender: Une marche avec Moïse (Psaumes 90)

Quatre disciplines oubliées qui transforment votre vie spirituelle

Dieu Parle Aussi La Nuit
