1
Mathayo 7:7
Biblia Habari Njema
BHN
“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata; bisheni mlango, nanyi mtafunguliwa.
Comparer
Explorer Mathayo 7:7
2
Mathayo 7:8
Maana, yeyote aombaye hupewa, atafutaye hupata, na abishaye mlango hufunguliwa.
Explorer Mathayo 7:8
3
Mathayo 7:24
“Kwa hiyo, kila mtu anayeyasikia maneno yangu na kuyazingatia, anafanana na mtu mwenye busara, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
Explorer Mathayo 7:24
4
Mathayo 7:12
“Yote mnayotaka watu wawatendee nyinyi, watendeeni wao vivyo hivyo. Hii ndiyo maana ya sheria ya Mose na mafundisho ya manabii.
Explorer Mathayo 7:12
5
Mathayo 7:14
Lakini njia inayoongoza kwenye uhai ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo.
Explorer Mathayo 7:14
6
Mathayo 7:13
“Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; waendao njia hiyo ni wengi.
Explorer Mathayo 7:13
7
Mathayo 7:11
Kama basi nyinyi, ingawa ni waovu, mwajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, hakika Baba yenu wa mbinguni atafanya zaidi: Atawapa mema wale wanaomwomba.
Explorer Mathayo 7:11
8
Mathayo 7:1-2
“Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu; kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu.
Explorer Mathayo 7:1-2
9
Mathayo 7:26
“Lakini yeyote anayesikia maneno yangu haya bila kuyazingatia, anafanana na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
Explorer Mathayo 7:26
10
Mathayo 7:3-4
Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako? Au, wawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi jichoni mwako,’ wakati wewe mwenyewe unayo boriti jichoni mwako?
Explorer Mathayo 7:3-4
11
Mathayo 7:15-16
“Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali. Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!
Explorer Mathayo 7:15-16
12
Mathayo 7:17
Basi, mti mzuri huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
Explorer Mathayo 7:17
13
Mathayo 7:18
Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
Explorer Mathayo 7:18
14
Mathayo 7:19
Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.
Explorer Mathayo 7:19