Soma Biblia Kila Siku 11/2024预览

Soma Biblia Kila Siku 11/2024

30天中的第16天

Daudi anaendelea kufunua hali yake inavyoonekana mbele ya wengine. Watu wengi, na hasa marafiki zake wanamwacha. Maadui zake wanatunga hila na fitina dhidi yake. Hata hivyo anavumilia lawama zote na fitina wanazofanya dhidi yake. Anajifanya kwamba hasikii wala hataki kuwajibu chochote. Anachofanya ni kutumia kinywa chake kumsifu Mungu badala ya kuwajibu maadui zake. Daudi anamua kuyaacha mambo yote mikononi mwa Mungu na kuamini kuwa shida na aibu yake itakwisha kwa sababu Mungu yu pamoja naye.

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 11/2024

Soma Biblia Kila Siku 11/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Kumi na moja pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Mathayo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More