Soma Biblia Kila Siku 11/2024预览

Soma Biblia Kila Siku 11/2024

30天中的第18天

Katika mwaka wa 12 wa utawala wa Ahazi huko Yuda, Hoshea alianza kutawala Samaria. Alifanya maovu mbele za Mungu. Waisraeli wakawa chini ya kongwa la mfalme wa Ashuru aliyewateka na kudai wampe kodi kila mwaka. Tunaonyeshwa kwamba dhambi dhidi ya Mungu ina madhara makubwa:Wakafuata ubatili, wakawa ubatili(m.15). Na Mungu alighadhabika sana, mpakahapana aliyesaliakati ya Waisraeli (m.18), kwa sababuhawakutaka kusikiaalipokuwa akiwaonya (m.14). Je, tunafanana nao?

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 11/2024

Soma Biblia Kila Siku 11/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Kumi na moja pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Mathayo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More