Soma Biblia Kila Siku 11/2024预览

Soma Biblia Kila Siku 11/2024

30天中的第11天

Suala la mshahara kwa mfuasi wa Yesu linaendelea kuwababaisha wanafunzi. Hasa ahadi ya Yesu kwamba watatawala naye katika ufalme wake. Nani ataonekana kuwa mkuu kati yao siku ile? Nani atakaa karibu zaidi na Yesu? Wana wa Zabedayo, yaani Yakobo na Yohana, walisaidiwa na mama yao. Lakini Yesu anakataa kabisa mawazo hayo. Nafasi ya kuwa mitume walipewa kwa neema. Wasiwe wanatumia nafasi hiyo kwa ajili ya kufikiria mambo ya cheo, bali watumie nguvu zao na mawazo yao kwa lengo la kuwatumikia wengine!

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 11/2024

Soma Biblia Kila Siku 11/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Kumi na moja pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Mathayo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More