Soma Biblia Kila Siku Mei 2021预览

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

31天中的第21天

Mara akawalazimisha wanafunzi wake (m.45). Kwa nini? Jana tuliona kuwa Yesu alitaka wapumzike baada ya kufanya kazi nyingi, lakini haikuwezekana kutokana na mkutano mkubwa uliowafuata. Hata hivyo baada ya kumaliza kusaidia mkutano huo, Yesu alizidi kusisitiza ni lazima wapumzike ili wapate nguvu mpya kimwili na kiroho. Vivyo hivyo kwa Yesu mwenyewe. Akaenda zake mlimani kuomba (m.46). Ndugu msomaji uliye mtumishi wa Bwana, tafadhali uzingatie sana fundisho hili la Yesu, usije ukadhoofika kimwili na kiroho na kumpa Shetani nafasi!

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ayubu. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu

More