Na tena Isaya anena,
Litakuwako shina la Yese,
Naye aondokeaye kuwatawala Mataifa;
Ndiye Mataifa watakayemtumaini.
Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu.