Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Tafuta matokeo ya: we all are sheep gone astray

Isa 53:6 (SUV)

Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na BWANA ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.

1 Pet 2:25 (SUV)

Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.

Lk 15:4 (SUV)

Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone?

Zab 23:1 (SUV)

BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

Zab 23:2 (SUV)

Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

Zab 23:3 (SUV)

Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

Zab 23:4 (SUV)

Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

Zab 23:5 (SUV)

Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.

Zab 23:6 (SUV)

Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.

Yn 10:11 (SUV)

Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.

Yn 10:14 (SUV)

Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;

Yer 50:6 (SUV)

Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea, wachungaji wao wamewapoteza; wamewapotosha milimani; wamekwenda toka mlima hata kilima, wamesahau mahali pao pa kupumzika.

Ebr 13:20 (SUV)

Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu Mchungaji Mkuu wa kondoo, kwa damu ya agano la milele, yeye Bwana wetu Yesu,

1 Pet 5:4 (SUV)

Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka.