Tafuta matokeo ya: Romans 3:23
Kol 3:23 (SUV)
Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, kama kwa Bwana, wala si kwa wanadamu,
Rum 3:23 (SUV)
kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
Gal 3:23 (SUV)
Lakini kabla ya kuja ile imani tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ije ile imani itakayofunuliwa.
Mwa 3:23 (SUV)
kwa hiyo BWANA Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.
Hes 3:23 (SUV)
Jamaa za Wagershoni watapanga rago nyuma ya maskani, upande wa magharibi.
Kum 3:23 (SUV)
Nikamnyenyekea BWANA wakati huo, nikamwambia,
Amu 3:23 (SUV)
Ndipo Ehudi akatoka nje barazani, akamfungia milango ya hicho chumba na kuifunga kwa ufunguo.
Neh 3:23 (SUV)
Baada yao wakafanyiza Benyamini na Hashubu, kuielekea nyumba yao. Baada yao akafanyiza Azaria, mwana wa Maaseya, mwana wa Anania, kando ya nyumba yake.
Ayu 3:23 (SUV)
Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukingo?
Mdo 3:23 (SUV)
Na itakuwa ya kwamba kila mtu asiyemsikiliza nabii huyo ataangamizwa na kutengwa na watu wake.
Isa 3:23 (SUV)
na vioo vidogo, na kitani nzuri, na vilemba, na utaji.
Omb 3:23 (SUV)
Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu.
Eze 3:23 (SUV)
Basi, nikaondoka, nikaenda uwandani, na tazama, utukufu wa BWANA ulisimama huko, kama utukufu ule niliouona karibu na mto Kebari; nami nikaanguka kifudifudi.
Mk 3:23 (SUV)
Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?
Dan 3:23 (SUV)
Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto.
Lk 3:23 (SUV)
Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,
Yn 3:23 (SUV)
Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na maji tele; na watu wakamwendea, wakabatizwa.
Mit 3:23 (SUV)
Ndipo utakapokwenda katika njia yako salama, Wala mguu wako hautakwaa.
Yer 3:23 (SUV)
Ni kweli, msaada haufai unaotazamiwa kutoka milimani, makutano yenye mshindo juu ya milima; ni kweli, wokovu wa Israeli ni katika BWANA, Mungu wetu.
2 Sam 3:23 (SUV)
Hata Yoabu, na jeshi lote waliokuwa pamoja naye, walipofika, watu wakamwambia Yoabu, wakisema, Abneri, mwana wa Neri, alikuja kwa mfalme, naye amemruhusu, naye amekwenda zake kwa amani.
1 Fal 3:23 (SUV)
Ndipo mfalme akasema, Huyu anasema, Mtoto wangu yu hai, na mtoto wako amekufa. Na huyu anasema, Sivyo hivyo; bali mtoto aliyekufa ni wako, na mtoto aliye hai ni wangu.
2 Fal 3:23 (SUV)
Wakasema, Ndiyo damu hii; bila shaka hao wafalme wameharibika, wamepigana kila mtu na mwenziwe; basi sasa, enyi Wamoabi, nyara hizo!
1 Nya 3:23 (SUV)
Na wana wa Nearia; Elioenai, na Hezekia, na Azrikamu, watu watatu.
1 Yoh 3:23 (SUV)
Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri.
1 Kor 3:23 (SUV)
nanyi ni wa Kristo, na Kristo ni wa Mungu.