Tafuta matokeo ya: Mathayo 6:33
Mt 6:33 (SUV)
Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.
Mt 6:34 (SUV)
Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
Mt 6:3 (SUV)
Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;
Mt 6:30 (SUV)
Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?
Mt 6:31 (SUV)
Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?
Mt 6:32 (SUV)
Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.
Mt 6:6 (SUV)
Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Mt 6:9 (SUV)
Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,
Mt 6:10 (SUV)
Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.
Mt 6:11 (SUV)
Utupe leo riziki yetu.
Mt 6:12 (SUV)
Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
Mt 6:13 (SUV)
Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]
Mt 6:21 (SUV)
kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.
Mt 6:25 (SUV)
Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
Mt 6:1 (SUV)
Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.
Mt 6:2 (SUV)
Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu.
Mt 6:4 (SUV)
sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Mt 6:5 (SUV)
Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
Mt 6:7 (SUV)
Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.
Mt 6:8 (SUV)
Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.
Mt 6:14 (SUV)
Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.
Mt 6:15 (SUV)
Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
Mt 6:16 (SUV)
Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.
Mt 6:17 (SUV)
Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;
Mt 6:18 (SUV)
ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.