Nembo ya Programu ya Biblia
Ikoni ya Utafutaji

Ufunuo 19:10 - Linganisha Matoleo Yote

Ufunuo 19:10 BHN (Biblia Habari Njema)

Basi, mimi nikaanguka kifudifudi mbele ya miguu yake, nikataka kumwabudu. Lakini yeye akaniambia, “Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako; sote tunamshuhudia Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio unaowaangazia manabii.”

Shirikisha
Ufunuo 19 BHN

Ufunuo 19:10 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)

Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.

Shirikisha
Ufunuo 19 SUV

Ufunuo 19:10 SRUV (Swahili Revised Union Version)

Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mtumishi mwenzako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.

Shirikisha
Ufunuo 19 SRUV

Ufunuo 19:10 NEN (Neno)

Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”

Shirikisha
Ufunuo 19 NEN