Yona 2:1-2 - Compare All Versions
Yona 2:1-2 BHN (Biblia Habari Njema)
Basi, Yona, akiwa tumboni mwa samaki huyo, akawa akimwomba Mwenyezi-Mungu, Mungu wake, akisema: “Kwa sababu ya taabu yangu, nilikuomba, ee Mwenyezi-Mungu, nawe ukanisikiliza; toka chini kuzimu, nilikulilia, nawe ukasikiliza kilio changu.
Yona 2:1-2 SRUV (Swahili Revised Union Version)
Ndipo Yona akamwomba BWANA, Mungu wake, akiwa katika tumbo la yule samaki, Akasema, Nilimlilia BWANA kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; Katika tumbo la kuzimu niliomba, Nawe ukasikia sauti yangu.
Yona 2:1-2 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Ndipo Yona akamwomba BWANA, Mungu wake, katika tumbo la yule samaki, Akasema, Nalimlilia BWANA kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; Katika tumbo la kuzimu naliomba, Nawe ukasikia sauti yangu.
Yona 2:1-2 NEN (Neno)
Akiwa ndani ya tumbo la samaki, Yona alimwomba BWANA Mungu wake. Akasema: “Katika shida yangu nalimwita BWANA, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu.