Yobu 14:7-9 - Compare All Versions
Yobu 14:7-9 BHN (Biblia Habari Njema)
Maana mti ukikatwa lipo tumaini la kuota, waweza kuchipua tena. Japo mizizi yake itazeeka udongoni, na shina lake kufia ardhini, lakini kwa harufu tu ya maji utachipua; utatoa matawi kama chipukizi.
Yobu 14:7-9 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka tena, Wala machipukizi yake hayatakoma. Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo; Lakini kwa harufu ya maji utachipuka, Na kutoa matawi kama mche.
Yobu 14:7-9 SRUV (Swahili Revised Union Version)
Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka tena, Wala machipukizi yake hayatakoma. Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo; Lakini kwa harufu ya maji utachipuka, Na kutoa matawi kama mche.
Yobu 14:7-9 NEN (Neno)
“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma. Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni, lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.