Yohane 4:1-4
Yohane 4:1-4 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza, (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake) aliondoka Yudea, akaenda zake tena mpaka Galilaya. Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.
Yohane 4:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)
Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane. (Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.) Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya; na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
Yohane 4:1-4 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza, (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake) aliondoka Yudea, akaenda zake tena mpaka Galilaya. Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.
Yohane 4:1-4 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza, (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,) aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya. Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.
Yohane 4:1-4 Neno: Bibilia Takatifu 2025 (NENO)
Yesu alipata habari kuwa Mafarisayo walisikia kwamba yeye alikuwa akipata wanafunzi kuliko Yohana na kuwabatiza, ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake. Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Yudea akarudi tena Galilaya. Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.