Yeremia 33:6-7 - Compare All Versions
Yeremia 33:6-7 BHN (Biblia Habari Njema)
“Hata hivyo, mimi nitauponya mji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama. Nitawastawisha tena watu wa Yuda na watu wa Israeli; nitawaimarisha kama walivyokuwa hapo awali.
Yeremia 33:6-7 SRUV (Swahili Revised Union Version)
Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli. Nami nitawarudisha wafungwa wa Yuda, na wafungwa wa Israeli, na kuwajenga kama kwanza.
Yeremia 33:6-7 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli. Nami nitawarudisha wafungwa wa Yuda, na wafungwa wa Israeli, na kuwajenga kama kwanza.
Yeremia 33:6-7 NEN (Neno)
“ ‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama. Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka uhamishoni, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.