Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ezra 5:3-4 - Compare All Versions

Ezra 5:3-4 BHN (Biblia Habari Njema)

Baadaye Tatenai, mtawala wa mkoa wa magharibi ya Eufrate, Shethar-bozenai na wenzao, walikwenda Yerusalemu na kuuliza, “Nani aliyewaamuru kuijenga nyumba hii mpaka kuimaliza?” Pia waliuliza, “Ni akina nani wanaojenga nyumba hii? Tunataka majina yao.”

Shirikisha
Ezra 5 BHN

Ezra 5:3-4 SRUV (Swahili Revised Union Version)

Wakati ule ule Tatenai, Mkuu wa mkoa wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzao, wakawajia, wakawaambia, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu? Ndipo wakawauliza hivi, Majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni gani?

Shirikisha
Ezra 5 SRUV

Ezra 5:3-4 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)

Wakati ule ule Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakawajia, wakawaambia, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu? Ndipo wakawauliza hivi, Majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani na nani?

Shirikisha
Ezra 5 SUV

Ezra 5:3-4 NEN (Neno)

Wakati ule Tatenai mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao waliwaendea, wakawauliza, “Ni nani aliyewapa ruhusa ya kujenga tena Hekalu hili na kurudishia upya kama lilivyokuwa?” Pia waliwauliza, “Je, majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani?”

Shirikisha
Ezra 5 NEN