Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

2 Wathesalonike 1:1-2 - Compare All Versions

2 Wathesalonike 1:1-2 BHN (Biblia Habari Njema)

Mimi Paulo, Silwano na Timotheo, kwa jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambayo ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.

2 Wathesalonike 1:1-2 SRUV (Swahili Revised Union Version)

Paulo, Silwano na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba yetu, na Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba, na kwa Bwana Yesu Kristo.

2 Wathesalonike 1:1-2 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)

Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba yetu, na Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba, na kwa Bwana Yesu Kristo.

2 Wathesalonike 1:1-2 NEN (Neno)

Paulo, Silvano na Timotheo. Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo. Neema na amani zinazotoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo ziwe nanyi.