Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 68:6-35

Zaburi 68:6-35 BHN

Mungu huwapa fukara makao ya kudumu, huwafungua wafungwa na kuwapa fanaka. Lakini waasi wataishi katika nchi kame. Ee Mungu, ulipowaongoza watu wako, uliposafiri kule jangwani, dunia ilitetemeka, mbingu zilitiririsha mvua; kwa kuweko kwako, Mungu wa Sinai, naam, kwa kuweko kwako, Mungu wa Israeli! Ee Mungu, uliinyeshea nchi mvua nyingi, uliiburudisha nchi yako ilipokuwa imechakaa. Watu wako wakapata humo makao; ukawaruzuku maskini kwa wema wako. Bwana alitoa amri, nao wanawake wengi wakatangaza habari: “Wafalme na majeshi yao wanakimbia ovyo!” Kina mama majumbani waligawana nyara, ingawa walibaki mazizini: Sanamu za njiwa wa madini ya fedha, na mabawa yao yanangaa kwa dhahabu. Mungu Mwenye Nguvu alipowatawanya wafalme huko, theluji ilianguka juu ya mlima Salmoni. Ewe mlima mrefu, mlima wa Bashani, ewe mlima wa vilele vingi, mlima wa Bashani! Mbona unauonea kijicho mlima aliochagua Mungu akae juu yake? Mwenyezi-Mungu atakaa huko milele! Akiwa na msafara mkubwa, maelfu na maelfu ya magari ya kukokotwa, Bwana anakuja patakatifuni pake kutoka Sinai. Anapanda juu akichukua mateka; anapokea zawadi kutoka kwa watu, hata kutoka kwa watu walioasi; Mwenyezi-Mungu apate kukaa huko. Mwenyezi-Mungu asifiwe siku kwa siku! Yeye hutubebea mizigo yetu; yeye ndiye Mungu wa wokovu wetu. Mungu wetu ni Mungu mwenye kutuokoa; Bwana Mungu pekee ndiye aokoaye katika kifo. Mungu ataviponda vichwa vya maadui zake, naam, vichwa vya wanaoshikilia njia mbaya. Bwana alisema: “Nitawarudisha maadui kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari, uoshe miguu katika damu ya maadui zako, nao mbwa wako wale shibe yao.” Ee Mungu, misafara yako ya ushindi yaonekana; misafara ya Mungu wangu, mfalme wangu, hadi patakatifu pake! Mbele waimbaji, nyuma wanamuziki, katikati wasichana wanavumisha vigoma. “Msifuni Mungu katika jumuiya kubwa ya watu. Msifuni Mwenyezi-Mungu, enyi wazawa wa Israeli!” Kwanza ni Benyamini, mdogo wa wote; kisha viongozi wa Yuda na kundi lao, halafu wakuu wa Zebuluni na Naftali. Onesha, ee Mungu, nguvu yako kuu; enzi yako uliyotumia kwa ajili yetu, kutoka hekaluni mwako, Yerusalemu, ambapo wafalme watakujia na zawadi zao. Uwakemee wale wanyama wakaao bwawani, kundi la mabeberu na fahali, mpaka mataifa hayo yakupe heshima na kodi. Uwatawanye hao watu wenye kupenda vita! Mabalozi watakuja kutoka Misri, Waethiopia watamletea Mungu mali zao. Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, mwimbieni Bwana nyimbo za sifa; mwimbieni yeye apitaye katika mbingu, mbingu za kale na kale. Msikilizeni akinguruma kwa kishindo. Itambueni nguvu kuu ya Mungu; yeye atawala juu ya Israeli, enzi yake yafika katika mbingu. Mungu ni wa kutisha patakatifuni pake, naam, yeye ni Mungu wa Israeli! Huwapa watu wake nguvu na enzi. Asifiwe Mungu!

Soma Zaburi 68

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 68:6-35

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha