Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

2 Mambo ya Nyakati UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu hiki cha pili cha Mambo ya Nyakati kinaendeleza masimulizi yale yaliyoachwa na kile cha kwanza; kinaanza kwa kueleza utawala wa Solomoni mpaka kufa kwake. Baada ya kusimulia juu ya uasi wa utawala wa makabila ya kaskazini chini ya Yeroboamu dhidi ya Rehoboamu mwanawe mfalme Solomoni na ambaye alitawala baada yake, kitabu kinaendelea hasa kusimulia habari za ufalme wa kusini wa Yuda mpaka wakati wa kuharibiwa mji wa Yerusalemu mnamo mwaka 586 K.K.
Aya za mwisho za kitabu hiki zinahusiana na vitabu vya Ezra na Nehemia na zinatualika kuendelea kusoma historia ya watu wa Israeli. Yamkini hapa mwishoni pana maneno yanayokariri tangazo alilotoa mfalme Koreshi ambalo liliwaruhusu Wayahudi kurudi makwao na kujenga upya hekalu la Yerusalemu. Tangazo hilohilo limeandikwa lote mwanzoni mwa kitabu cha Ezra.

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha