Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 73:13-28

Zaburi 73:13-28 SRUV

Hakika nimejisafisha moyo wangu bure, Na kunawa mikono yangu nisitende dhambi. Maana mchana kutwa nimepigwa, Na kuadhibiwa kila asubuhi. Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo; Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako. Nami nilifikiri jinsi ya kufahamu hayo; Ikawa taabu machoni pangu; Hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu, Nikautafakari mwisho wao. Hakika Wewe huwaweka penye utelezi, Huwaangusha mpaka palipoharibika. Namna gani wameangamizwa punde! Wakafutiliwa mbali kwa vitisho. Ee Bwana, wamekuwa kama ndoto wakati wa kuamka, Uondokapo utaidharau sanamu yao. Moyo wangu ulipoona uchungu, Viuno vyangu viliponichoma, Nilikuwa kama mjinga, sijui neno; Nilikuwa kama mnyama tu mbele zako. Walakini mimi ni pamoja nawe daima, Umenishika mkono wa kulia. Utaniongoza kwa shauri lako, Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu. Ni nani niliye naye mbinguni, Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe. Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele. Maana wajitengao nawe watapotea; Umewaangamiza wote waliokuacha Wewe. Nami kumkaribia Mungu ni kwema kwangu; Nimefanya kimbilio kwa Bwana MUNGU, Niyahubiri matendo yako yote.

Soma Zaburi 73