Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 38:1-10

Zaburi 38:1-10 SRUV

Ee BWANA, usinilaumu katika ghadhabu yako, Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako. Kwa maana mishale yako imenichoma, Na mkono wako umenipata. Hamna uzima katika mwili wangu Kwa sababu ya ghadhabu yako. Wala hamna amani mifupani mwangu Kwa sababu ya hatia zangu. Maana dhambi zangu zimenifunika kichwa, Kama mzigo mzito zimenilemea mno. Majeraha yangu yananuka na kutunga usaha, Kwa sababu ya upumbavu wangu. Nimejipinda na kuinama sana, Mchana kutwa ninaenda nikiomboleza. Maana viuno vyangu vimejaa homa, Wala hamna uzima katika mwili wangu. Nimedhoofika na kupondeka sana, Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu. Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako, Kuugua kwangu hakukusitirika kwako. Moyo wangu unadundadunda, Nguvu zangu zimenitoka; Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.

Soma Zaburi 38