Luka 18:15-17
Luka 18:15-17 SRUV
Wakamletea na watoto wachanga ili awaguse; lakini wanafunzi walipoona waliwakemea. Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao. Amin, nawaambia, Mtu yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe.