Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 21:1-11

Kutoka 21:1-11 SRUV

Basi hukumu utakazoziweka mbele ya watu ni hizi Ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia muda wa miaka sita; mwaka wa saba atatoka kwako huru bure. Ikiwa aliingia kwako peke yake tu, atatoka hivyo peke yake; kama ameoa, mkewe atatoka aende pamoja naye. Ikiwa ni bwana wake aliyemwoza huyo mke, naye amemzalia wana, wa kiume au wa kike; yule mke na wanawe watakuwa ni mali ya bwana wake, naye mume atatoka peke yake. Lakini huyo mtumwa akisema waziwazi, Mimi nampenda bwana wangu, na mke wangu na watoto wangu; sitaki mimi kutoka niwe huru; ndipo hapo huyo bwana wake atamleta mbele ya Mungu na kumleta mlangoni, au penye mwimo wa mlango; na bwana wake atalitoboa sikio lake kwa uma; ndipo atamtumikia sikuzote. Mtu akimwuza binti yake awe kijakazi, hatatoka yeye kama watumwa wa kiume watokavyo. Ikiwa bwana wake hakupendezewa naye, akiwa amemposa, ndipo atakubali akombolewe; hana amri yeye kumwuza aende kwa watu wageni maana amemtenda kwa udanganyifu. Akimposa mwanawe, atamtendea kama desturi zipasazo binti zake. Akijitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia. Ikiwa hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali.

Soma Kutoka 21