Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 56

56
Kumtumaini Mungu katika Mateso
Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Njiwa Mkimya wa Mbali. Utenzi wa Daudi alipokamatwa na Wafilisti kule Gathi.
1 # Zab 31:9 Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza,
Mchana kutwa ananionea akileta vita.
2 # Zab 57:3 Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa,
Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi.
3 # 1 Sam 30:6; 2 Nya 20:3 Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;
4 # Ebr 13:5,6 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake.
Nimemtumaini Mungu, sitaogopa;
Mwenye mwili atanitenda nini?
5Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu,
Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya.
6 # Mdo 4:27,28 Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu,
Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.
7Je! Wataokoka kwa uovu wao?
Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.
8 # Mal 3:16 Umehesabu kutanga-tanga kwangu;
Uyatie machozi yangu katika chupa yako;
(Je! Hayamo katika kitabu chako?)
9 # Isa 8:9,10 Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo.
Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu;
10Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake.
Kwa msaada wa BWANA nitalisifu neno lake.
11Nimemtumaini Mungu, sitaogopa;
Mwanadamu atanitenda nini?
12 # Zab 116:14-16 Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu;
Nitakutolea dhabihu za kushukuru.
13 # Ayu 33:30 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti;
Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke?
Ili nienende mbele za Mungu
Katika nuru ya walio hai.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 56: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha