Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 43

43
Sala kwa Mungu Wakati wa Shida
1 # Zab 7:8 Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki,
Uniokoe na mtu wa hila asiye haki.
2 # Zab 28:7; Isa 26:4 Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa?
Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?
3 # Zab 2:6; 3:4 Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze,
Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata maskani yako.
4Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye
furaha yangu na shangwe yangu;
Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.
5 # Zab 42:5,11 Nafsi yangu, kwa nini kuinama,
Na kufadhaika ndani yangu?
Umtumaini Mungu;
Kwa maana nitakuja kumsifu,
Aliye afya ya uso wangu,
Na Mungu wangu.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 43: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha