Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 3

3
Mwamini Mungu katika Dhiki
Zaburi ya Daudi alipomkimbia mwanawe, Absalomu.
1 # 2 Sam 15:13—17:22 BWANA, watesi wangu wamezidi kuwa wengi,
Ni wengi wanaonishambulia,
2 # 2 Sam 16:8; Zab 22:7,8 Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu,
Hana wokovu huyu kwa Mungu.
3 # 2 Fal 25:27; Zab 27:6 Na Wewe, BWANA, U ngao yangu pande zote,
Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.
4Kwa sauti yangu namwita BWANA
Naye aniitikia toka mlima wake mtakatifu.
5 # Zab 4:8; Mit 3:24; Mdo 12:6 Nalijilaza nikalala usingizi, nikaamka,
Kwa kuwa BWANA ananitegemeza.
6Sitayaogopa makumi elfu ya watu,
Waliojipanga juu yangu pande zote.
7BWANA, uinuke, Mungu wangu, uniokoe,
Maana umewapiga taya adui zangu wote;
Umewavunja meno wasio haki.
8 # Zab 37:39,40; Mit 21:31; Hes 13:4 Wokovu una BWANA;
Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 3: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha