Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 148

148
Sifa kwa Utukufu Mkuu wa Mungu
1Haleluya.
Msifuni BWANA kutoka mbinguni;
Msifuni katika mahali palipo juu.
2 # Dan 7:10; Ebr 1:7 Msifuni, enyi malaika wake wote;
Msifuni, majeshi yake yote.
3Msifuni, jua na mwezi;
Msifuni, nyota zote zenye mwanga.
4 # 1 Fal 8:27 Msifuni, enyi mbingu za mbingu,
Nanyi maji mlioko juu ya mbingu.
5 # Ebr 11:3 Na vilisifu jina la BWANA,
Kwa maana aliamuru, vikaumbwa.
6 # Yer 33:25 Amevithibitisha hata milele na milele,
Ametoa amri wala haitapita.
7 # Isa 43:20 Msifuni BWANA kutoka nchi,
Enyi nyangumi na vilindi vyote.
8Moto na mvua ya mawe, theluji na mvuke,
Upepo wa dhoruba ulitendao neno lake.
9 # Isa 49:13 Milima na vilima vyote,
Miti yenye matunda na mierezi yote.
10Hayawani, na wanyama wafugwao,
Vitambaavyo, na ndege wenye mbawa.
11 # Mdo 17:28 Wafalme wa dunia, na watu wote,
Wakuu, na makadhi wote wa dunia.
12Vijana waume, na wanawali,
Wazee, na watoto;
13 # Isa 6:3; Flp 2:9 Na walisifu jina la BWANA,
Maana jina lake peke yake limetukuka;
Adhama yake i juu ya nchi na mbingu.
14 # Efe 2:17; 1 Pet 2:9 Naye amewainulia watu wake pembe,
Sifa za watauwa wake wote;
Wana wa Israeli, watu walio karibu naye.
Haleluya.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 148: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha