Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 146

146
Sifa kwa Kupata Msaada wa Mungu
1Haleluya.#146:1Haleluya maana yake ni, Msifuni BWANA.
Ee nafsi yangu, umsifu BWANA.
2Nitamsifu BWANA muda ninaoishi,
Nitamwimbia Mungu wangu ningali ni hai.
3 # Isa 2:22 Msiwatumainie wakuu,
Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.
4 # Mhu 12:7; 1 Kor 2:6 Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake,
Siku hiyo mawazo yake yapotea.
5 # Yer 17:7 Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,
Na tumaini lake ni kwa BWANA, Mungu wake,
6 # Mik 7:20; Mdo 4:24; 14:15; Ufu 14:7 Aliyezifanya mbingu na nchi,
Bahari na vitu vyote vilivyomo.
Huishika kweli milele,
7Huwafanyia hukumu walioonewa,
Huwapa wenye njaa chakula;
BWANA hufungua waliofungwa;
8BWANA huwafumbua macho waliopofuka;
BWANA huwainua walioinama;
BWANA huwapenda wenye haki;
9BWANA huwahifadhi wageni;
Huwategemeza yatima na mjane;
Bali njia ya wasio haki huipotosha.
10BWANA atamiliki milele,
Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi hata kizazi.
Haleluya.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 146: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha