Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 137

137
Maombolezo juu ya Maangamizi ya Yerusalemu
1 # Eze 1:1; Dan 8:2; Isa 24:8; Omb 5:15; Amo 8:10; Ufu 18:22 Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,
Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2Katika miti iliyo katikati yake
Tulivitundika vinubi vyetu.
3Maana huko waliotuchukua mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea walitaka furaha;
Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4Tuuimbeje wimbo wa BWANA
Katika nchi ya ugeni?
5Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe,
Mkono wangu wa kuume na usahau.
6 # Eze 3:26 Ulimi wangu na ugandamane
Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
7 # Omb 4:22; Oba 1:10 Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,
Siku ya Yerusalemu.
Waliosema, Bomoeni!
Bomoeni hata misingini!
8 # Isa 13:1; Ufu 18:6 Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,
Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
9Heri yeye atakayewakamata wadogo wako,
Na kuwaseta wao juu ya mwamba.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 137: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha