Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 116

116
Shukrani kwa Kuponywa Maradhi
1Haleluya.
Nampenda BWANA kwa kuwa anaisikiliza
Sauti yangu na dua zangu.
2Kwa maana amenitegea sikio lake,
Kwa hiyo nitamwita siku zangu zote.
3Kamba za mauti zilinizunguka,
Shida za kuzimu zilinipata.
Naliona taabu na huzuni;
4Nikaliitia jina la BWANA.
Ee BWANA, nakuomba sana,
Uniokoe nafsi yangu.
5 # Ezr 9:15; Neh 9:8; Zab 11:7; Yer 12:1; Omb 1:18; Ufu 16:5 BWANA ni mwenye neema na haki,
Naam, Mungu wetu ni mwenye rehema.
6BWANA huwalinda wasio na hila;
Nalidhilika, akaniokoa.
7 # Yer 6:16; Mt 11:29 Ee nafsi yangu, urudi rahani mwako,
Kwa kuwa BWANA amekutendea ukarimu.
8Maana umeniponya nafsi yangu na mauti,
Macho yangu na machozi,
Na miguu yangu na kuanguka.
9Nitaenenda mbele za BWANA
Katika nchi za walio hai.
10 # 2 Kor 4:13 Naliamini, kwa maana nitasema,
Mimi naliteswa sana.
11 # 2 Fal 4:16; Yer 9:5; Rum 3:4 Mimi nalisema kwa haraka yangu,
Wanadamu wote ni waongo.
12Nimrudishie BWANA nini
Kwa ukarimu wake wote alionitendea?
13Nitakipokea kikombe cha wokovu;
Na kulitangaza jina la BWANA;
14 # Zab 22:25; Yon 2:6 Nitaziondoa nadhiri zangu kwa BWANA,
Naam, mbele ya watu wake wote.
15 # Ayu 5:26; Zab 72:14; Lk 16:22; Ufu 14:13 Ina thamani machoni pa BWANA
Mauti ya wacha Mungu wake.
16Ee BWANA, hakika mimi ni mtumishi wako,
Mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako,
Umevifungua vifungo vyangu.
17Nitakutolea dhabihu ya kushukuru;
Na kulitangaza jina la BWANA;
18Nitaziondoa nadhiri zangu kwa BWANA,
Naam, mbele ya watu wake wote.
19Katika nyua za nyumba ya BWANA,
Ndani yako, Ee Yerusalemu.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 116: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha