Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 11

11
Wimbo wa Kumtumainia Mungu
Kwa mwimbishaji. Ya Daudi.
1BWANA ndiye niliyemkimbilia.
Mbona mnaiambia nafsi yangu,
Kimbia kama ndege mlimani kwenu?
2Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta,
Wanaitia mishale yao katika upote,
Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
3Kama misingi ikiharibika,
Mwenye haki atafanya nini?
4 # Hab 2:20; Efe 5:13; Ebr 4:13 BWANA yu katika hekalu lake takatifu.
BWANA ambaye kiti chake kiko mbinguni,
Macho yake yanaangalia;
Kope zake zinawajaribu wanadamu.
5 # Ayu 5:17; Zab 94:12 BWANA humjaribu mwenye haki;
Bali nafsi yake humchukia asiye haki,
Na mwenye kupenda udhalimu.
6Awanyeshee wasio haki mitego,
Moto na kiberiti na upepo wa hari,
Na viwe fungu la kikombe chao.
7Kwa kuwa BWANA ndiye mwenye haki,
Apenda matendo ya haki,
Wanyofu wa moyo watamwona uso wake.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 11: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha