Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isa 12

12
Shukrani na Sifa
1 # Isa 2:11; Zek 14:20,21 Na katika siku hiyo utasema,
Ee BWANA, nitakushukuru wewe;
Kwa kuwa ijapokuwa ulinikasirikia,
Hasira yako imegeukia mbali,
Nawe unanifariji moyo.
2 # Kut 15:2; Zab 118:14 Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu;
Nitatumaini wala sitaogopa;
Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu;
Naye amekuwa wokovu wangu.
3 # Yer 2:13; Yn 4:10,14 Basi, kwa furaha mtateka maji katika visima vya wokovu. 4Na katika siku hiyo mtasema,
Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake;
Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa,
Litajeni jina lake kuwa limetukuka.
5Mwimbieni BWANA; kwa kuwa ametenda makuu;
Na yajulikane haya katika dunia yote.
6 # Isa 54:1; Sef 3:14; Lk 19:37-40 Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni;
Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako.

Iliyochaguliwa sasa

Isa 12: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha