Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Sefania Utangulizi

Utangulizi
Maana ya Sefania ni “Aliyefichwa na Yehova.” Alikuwa wa ukoo wa Hezekia, mfalme wa Yuda. Nabii Sefania alihudumu wakati wa utawala wa Mfalme Yosia. Sefania alionya kwamba siku ya Bwana ingeleta hukumu kwa Yuda pamoja na Yerusalemu, hivyo akawashauri Wayahudi kumrudia Mungu. Uvamizi wa kuteka Yuda ulikuwa unakuja kutoka kaskazini, nao ungekumba pia mataifa yaliyowazunguka. Ingawa hukumu ya Yuda imeainishwa, ahadi ya kufanywa upya ni yakini. Mataifa yatahukumiwa na kutiishwa na mfalme wa Israeli, atakayetawala kutoka Sayuni.
Mwandishi
Sefania.
Kusudi
Kuwaonya watu wa Yuda waepukane na kuabudu sanamu na wamrudie Mungu wao.
Mahali
Yerusalemu.
Tarehe
Kati ya 640–621 K.K.
Wahusika Wakuu
Sefania, na watu wa Yuda.
Wazo Kuu
Sefania aliwapa watu matumaini kwamba Mungu angewarudisha watu wake nyumbani.
Mambo Muhimu
Hukumu juu ya Yuda na mataifa ya Wafilisti, Amoni na Moabu. Yerusalemu pia inatajwa kwa siku zijazo.
Mgawanyo
Kutangazwa kwa hukumu ya Mungu (1:1–2:3)
Hukumu dhidi ya mataifa (2:4-15)
Maisha ya baadaye ya Yerusalemu (3:1-20).

Iliyochaguliwa sasa

Sefania Utangulizi: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha