Zaburi 3
3
Zaburi 3
Sala ya asubuhi ya kuomba msaada
Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu.
1Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi!
Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
2Wengi wanasema juu yangu,
“Mungu hatamwokoa.”
3Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao yangu pande zote;
umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
4Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu,
naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
5Ninajilaza na kupata usingizi;
naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
6Sitaogopa makumi elfu ya adui,
wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
7Ee Bwana, amka!
Niokoe, Ee Mungu wangu!
Wapige adui zangu wote kwenye taya,
vunja meno ya waovu.
8Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana.
Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 3: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.