Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 147

147
Zaburi 147
Kumsifu Mungu wa majeshi
1Msifuni Bwana.#147:1 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah; pia 147:20.
Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa,
jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!
2 Bwana hujenga Yerusalemu,
huwakusanya Israeli walio uhamishoni.
3Anawaponya waliovunjika mioyo
na kuvifunga vidonda vyao.
4Huzihesabu nyota
na huipa kila moja jina lake.
5Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi,
ufahamu wake hauna kikomo.
6 Bwana huwahifadhi wanyenyekevu
lakini huwashusha waovu hadi mavumbini.
7Mwimbieni Bwana kwa shukrani,
mpigieni Mungu wetu kinubi.
8Yeye huzifunika anga kwa mawingu,
huinyeshea ardhi mvua,
na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima.
9Huwapa chakula mifugo
na pia makinda ya kunguru yanapolia.
10Furaha yake haipo katika nguvu za farasi,
wala furaha yake kwenye miguu ya shujaa.
11 Bwana hupendezwa na wale wamchao,
wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma.
12Mtukuze Bwana, ee Yerusalemu,
msifu Mungu wako, ee Sayuni,
13kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako
na huwabariki watu wako walio ndani yako.
14Huwapa amani mipakani mwenu
na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.
15Hutuma amri yake duniani,
neno lake hukimbia kasi.
16Anatandaza theluji kama sufu
na kutawanya umande kama majivu.
17Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe.
Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
18Hutuma neno lake na kuviyeyusha,
huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.
19Amemfunulia Yakobo neno lake,
sheria zake na maagizo yake kwa Israeli.
20Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote,
hawazijui sheria zake.
Msifuni Bwana.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 147: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia