Zaburi 137
137
Zaburi 137
Maombolezo ya Israeli uhamishoni
1Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza
tulipokumbuka Sayuni.
2Kwenye miti ya huko
tulitundika vinubi vyetu,
3kwa maana huko hao waliotuteka
walitaka tuwaimbie nyimbo;
watesi wetu walidai nyimbo za furaha;
walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja
kati ya nyimbo za Sayuni!”
4Tutaimbaje nyimbo za Bwana,
tukiwa nchi ya kigeni?
5Nikikusahau wewe, ee Yerusalemu,
basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu
kama sitakukumbuka wewe,
kama nisipokufikiri Yerusalemu
kuwa furaha yangu kubwa.
7Kumbuka, Ee Bwana, walichokifanya Waedomu,
siku ile Yerusalemu ilipoanguka.
Walisema, “Bomoa, bomoa
hata misingi yake!”
8Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa,
heri yeye atakayekulipiza wewe
kwa yale uliyotutenda sisi:
9yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga
na kuwaponda juu ya miamba.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 137: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.