Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 120

120
Zaburi 120
Kuomba msaada dhidi ya wadanganyifu
Wimbo wa kwenda juu.
1Katika dhiki yangu namwita Bwana,
naye hunijibu.
2Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo
na ndimi za udanganyifu.
3Atakufanyia nini,
au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,
kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,
kwamba naishi katikati ya mahema ya Kedari!
6Nimeishi muda mrefu mno
miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7Mimi ni mtu wa amani;
lakini ninaposema, wao wanataka vita.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 120: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia